Mhandisi Mshauri atakiwa kusimamia vizuri ili mradi wa maji wa miji 28 ukamilike kwa wakati.

Mkurugenzi Sera na Mipango Wizara ya Maji Prosper Buchafwe akiwasilisha taarifa kwa Niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji Profesa Jamal Katundu

Prosper Buchafwe. Mkurugenzi Sera na Mipango, Wizara ya Maji


 

Katibu Mkuu Wizara ya Maji Prof. Jamal Katundu amemtaka Mhandisi Mshauri kampuni ya Management Consultant (MC) kuhakikisha wanatoa ushauri wenye tija ili mradi wa maji wa miji 28 utekelezwe na kukamilika kwa wakati.

Agizo hilo amelitoa leo jijini Dodoma kupitia taarifa yake iliyosomwa na Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Wizara ya Maji Prosper Buchafwe wakati wa kikao  kuhusu utekelezaji wa mradi wa maji wa miji 28 kilichofanyika Dodoma.

Prof.Katundu amesema wananchi wanahitaji majisafi, salama na yenye kutosheleza hivyo Mhandisi mshauri anajukumu la kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa kuzingatia viwango na ukamilike katika muda uliopangwa na kwamba hilo litawezekana iwapo watakuwa washauri wazuri kwa Menejimenti ya Wizara ili  kufanya maamuzi yenye tija.

Ameishukuru Serikali ya India kwa kuwezesha kupatikana kwa fedha za utekelezaji wa mradi huo ambao utapunguza kwa kiasi kikubwa changamoto ya huduma ya maji katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Mradi wa maji wa miji 28 umefadhiliwa na serikali ya India kupitia mkopo wenye masharti nafuu wa dola milioni 500 sawa na zaidi ya shilingi trilioni moja za Tanzania ambazo zitafanikisha mradi huo

Comments

Popular posts from this blog

Ujenzi wa Mabwawa kusaidia kuondoa changamoto ya maji Dodoma

Wataalamu Sekta ya maji shirikishaneni maarifa – Naibu Waziri Maji

Katibu Mkuu Wizara ya Maji asisitiza matumizi ya mfumo wa taarifa za sekta ya maji (Maji App)