Serengeti waomba huduma ya maji toka ziwa Victoria

Naibu katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kumaliza kukagua mradi wa maji Serengeti

Mbunge wa Jimbo la Serengeti Mhe. Dkt. Amsabi Mrimi akizungumza wakati wa Ziara ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Cyprian Luhemeja
Naibu Katibu Mkuu Mhandisi Cyprian Luhemeja akikagua mradi wa maji Mugumu
Chujio la maji Mugumu
Bwawa la Manchira lililoko Wilayani Serengeti

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Cyprian Luhemeja amewaagiza wataalam wa Wizara wa Maji kufanya utafiti ndani ya siku tatu wawasilishe taarifa ya namna bora ya kuwezesha upatikanaji endelevu wa huduma ya maji kwa wananchi wa Serengeti.

Ametaka taarifa hiyo baada ya kupokea maelezo ya Mbunge wa jimbo hilo Mhe. Dkt. Amsabi Mrimi  kuwa kina cha maji kimepungua kwenye bwawa la Manchira ambalo ni chanzo cha maji cha mradi wa maji wa Mugumu ambao unatarajiwa kuhudumia wakazi wa eneo hilo.

Luhemeja amesema utekekezaji wa mradi huo unaruhusu kusanifu na kujenga hivyo wataalam waje na ushauri iwapo kuna umuhimu wa mradi huo kutumia maji ya Ziwa victoria kupitia mradi wa Tarime-Rorya ambao utekekezaji wake unaendelea.

"Katika Wilaya ya Serengeti wananchi wanatumia maji kutoka bwawa la Manchira kama chanzo cha maji, lakini Mheshimiwa Mbunge anaonesha wasiwasi kwamba inawezekana bwawa hili lisiwe chanzo endelevu kutoa huduma katika eneo hili kutokana na mabadiliko ya tabianchi yanayoathiri ujazo wa maji" Mhandisi Luhemeja amesema

Mhandisi Luhemeja ametoa wito kwa wananchi wa Serengeti kutunza vyanzo vya maji Ili kupunguza athari zinazoweza kukumba vyanzo hivyo.

Aidha Mhe. Dkt. Amsabi ameshukuru Serikali ya awamu ya Sita kwa kutenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 20 kuboresha huduma ya maji katika Wilaya ya Serengeti.

"Ongezeko la watu katika Mji huu ni kubwa sana, utalii unakua kwa kasi na maji yanahitajika sana, chanzo tulichonacho kwa sasa bwawa la Manchira limezidi kupungua maji kutoka mita tisa mpaka sita tangu lilipotengenezwa, ni muda sasa wananchi hawa wakapata maji kutoka ziwa Victoria ambacho ni chanzo cha uhakika" Mhe Mrimi ameomba

Mhandisi Wiston Agwaro Kaimu Afisa Maji kutoka Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria ameeleza kuwa chanzo cha maji cha Bwawa la Manchira kinatosheleza kwa mahitaji ya sasa.

Amekili kuwepo na changamoto ya mabadiliko ya tabianchi ambayo yanasababisha kupungua kwa maji

Comments

Popular posts from this blog

Ujenzi wa Mabwawa kusaidia kuondoa changamoto ya maji Dodoma

Wataalamu Sekta ya maji shirikishaneni maarifa – Naibu Waziri Maji

Katibu Mkuu Wizara ya Maji asisitiza matumizi ya mfumo wa taarifa za sekta ya maji (Maji App)