Katibu Mkuu Maji awataka 'Maji Sport' kuleta vikombe mashindano ya SHIMIWI

 

Picha ya pamoja ya viongozi wa Maji Sport na Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga

Katibu wa Maji Sport James Kalumanzila akimkabidhi Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga zawadi ya jezi ya Maji Sport
Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga

Viongozi wa Klabu ya Michezo ya Wizara ya Maji (Maji Sports Club) wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Club hiyo Andrew Rutta wamefika ofisini kwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga kwa dhumuni la kujitambulisha na kumpa maendeleo ya Klabu hiyo.

Katibu Mkuu Amewapongeza kwa utayari wao wa kushiriki mashindano. Amesisitiza kuwa suala la michezo ni muhimu kwa Wizara ya Maji ambayo ina jukumu la kuwapelekea wananchi huduma ya majisafi na salama. Michezo inasaidia kuleta umoja, afya na inajenga uzalendo na mshikamano.

Amewataka washiriki wawe na nidhamu ili kufikia lengo lililokusudiwa, wasiwagawe watumishi, michezo isiwe uadui iwe ni furaha na kujenga umoja na mshikamano uliokusudiwa.

Klabu ya Maji inajiandaa kwa ajili ya mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Taasisi za Serikali (SHIMIWI) yanayotarajiwa kufanyika Jijini Tanga kuanzia Agost 1, mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

Ujenzi wa Mabwawa kusaidia kuondoa changamoto ya maji Dodoma

Wataalamu Sekta ya maji shirikishaneni maarifa – Naibu Waziri Maji

Katibu Mkuu Wizara ya Maji asisitiza matumizi ya mfumo wa taarifa za sekta ya maji (Maji App)