Kongamano la Kisayansi la Kimataifa kufanyika Dar Es Salaam

Mkuu wa Chuo cha Maji Dkt. Adam Karia akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na Kongamano la Kisayansi la Maji linalotarajiwa kufanyikia kwa siku mbili kuanzia kesho Aprili 4-5 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Mgeni Rasmi katika kongamano hilo ni Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi.

Dkt. Karia amesema wadau wa sekta ya maji zaidi ya 400 kutoka sehemu mbalimbali Duniani wanatarajia kushiriki. Aidha, matokeo ya tafiti zaidi ya 60 zenye lengo la kuleta matokeo chanya katika kutatua changamotop za sekta ya maji nchini zinatarajiwa kuwasilishwa.




 

Comments

Popular posts from this blog

Ujenzi wa Mabwawa kusaidia kuondoa changamoto ya maji Dodoma

Wataalamu Sekta ya maji shirikishaneni maarifa – Naibu Waziri Maji

Katibu Mkuu Wizara ya Maji asisitiza matumizi ya mfumo wa taarifa za sekta ya maji (Maji App)